Mjasiriamali: Utengenezaji wa mafuta ya mgando (ya kupaka)

PamojaForums · Sep 6, 2026 at 1:53 AMReplies 0 · Views 0
#1
Habari wana JF...

Tujifunze utengeneza wa mafuta ya mgando.


MALIGHAFI

1. MICRO WAX

2. WHITE OIL

3. RANGI

4. PERFUME

5. VIFUNGASHIO


JINSI YA KUTENGENEZA


Weka MICRO WAX kilo 1 kwenye sufuria kisha injika jikoni, ikianza kuyeyuka miminia WHITE OIL lita 2 weka RANGI nusu kijiko cha chai kama utapenda.


Ipua kisha weka PERFUME (MANUKATO) kijiko kimoja cha chakula kama utapenda. Acha yaanze kupoa, yakianza kuwa mazito paki kwenye VIFUNGASHIO. Yakiganda funga vifungashio tumia au kauze.


Asante...

-Queen Chagga


 
No reactions yetReply / React
Continue the discussion on PamojaForumsOpen full thread