Kichaa cha mbwa (Rabies)

PamojaForums · Sep 6, 2026 at 11:08 AMReplies 0 · Views 4
#1
KICHAA CHA MBWA


Ugonjwa hatari unaopuuzwa sana hasa katika nchi masikini. Ugonjwa huu pia unatatizo la kutotolewa taarifa kamili. Kwa nchi kama Tanzania ugonjwa huu unaonekana kama kaugonjwa kadogo sana. Unaua zaidi ya kipindupindu, unaua karibu ya HIV. Ugonjwa huu unaua zaidi nguvu kazi maana unaua watoto zaidi.


Ugonjwa huu haupo kabisa nchi nyingi za ulaya. Hata marekani ugonjwa huu hauwapati watu maana wanyama wanachanjwa.


Kuchanja (vaccination) ndiyo njia bora na rahisi ya kuzuia ugonjwa huu. Napenda kuwataarifu Watanzania wenzangu kuchanja mbwa wao pamoja na paka ili tuweze kuzuia huu ugonjwa.


 
No reactions yetReply / React
Continue the discussion on PamojaForumsOpen full thread