Cheka Time ya VodaCom ni utapeli

PamojaForums · Sep 6, 2026 at 11:07 AMReplies 0 · Views 0
#1
Nikiwa mteja maarufu na mtumiaji mzuri wa huduma toka Vodacom napata simanzi pale tunapotangaziwa kuwa ukijisajili kupata huduma hii (yaani ukiandika *147*07#) utakatwa shilingi 500 na kupata dakika 60 za kuongea BURE voda kwenda voda siku nzima.


Sasa tukija kwenye reality utaona mtu unapewa dakika hizo 60 za kuongea bure kuanzia saa 12 asubuhi au time yoyote mchana mpaka saa 12 jioni huduma inakwisha.


Ukisikiliza matangazo yao wanasema huduma hii inadumu kwa masaa 24. Wakati reality inaishia saa 12 jioni


Sasa hapo ndipo tunapo ona jamaa zetu wanaTUTAPELI. Sasa tunaomba wawe wawazi waseme ukweli.


Bila shaka humu wamo watueke wazi.


 
No reactions yetReply / React
Continue the discussion on PamojaForumsOpen full thread